Na Mwandishi Maalumu
Rais
wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,
Jumatatu, Juni 30, 2014, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka
kampuni ya simu ya Viettel kutoka Vietnam ukiongozwa na Le Dang Dung ambaye ni Makamu wa Rais wa Kundi
la makampuni ya Viettel Group.
Kwenye
mkutano huo uliofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, Le Dung amefuatana na Tao Duc
Thang ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Shughuli za Kimataifa za Kampuni hiyo –
Viettel Global.
Dung amemwelezea Rais Kikwete kuhusu mipango
ya Viettel kuwekeza katika shughuli ya mawasiliano ya simu hasa kwa maeneo ya
vijijini.
No comments:
Post a Comment