Sunday, June 22, 2014

RAIS JAKAYA KIKWETE AKUTANA NA MJUMBE WA KAMATI TENDAJI YA CHAMA TAWALA CHA CHINA




Na Mwandishi Maalumu

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumapili, Juni 22, 2014, amekutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Anne Wu Suk Ching, Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Chama Tawala cha Jamhuri ya Watu wa China.

 Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete na Mheshimiwa Anne Ching wamejadili hali ya uhusiano kati ya Tanzania na China na jinsi nchi hizo mbili zinavyoweza kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo ulioanzishwa miaka 50 iliyopita.

Dkt. Anne Ching pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Vituo vya Biashara Duniani, Tawi la Hong Kong (World Trade Centre Association Honk Kong) na pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Biashara ya China na Afrika, Tawi la Hong Kong (China-Africa Business Coundil Hong Kong Chapter).

Rais Kikwete pia amepokea ujumbe maalum kutoka kwa Mfalme Qaboos Bin Said wa Oman uliowasilishwa na mjumbe maalum wa kiongozi huyo, Mheshimiwa Masoud Mohamed Al-Ruqaishi, ambaye pia ni Balozi wa Oman katika Tanzania.
Baada ya kupokea ujumbe huo, Rais Kikwete amemwomba Balozi huyo kuwasilisha shukurani zake kwa Mfalme Qaboos kwa ujumbe huo maalum.

No comments:

Post a Comment