Tuesday, February 18, 2014

matukio mbalimbali ya makabidiano ya benki ya NMB pamoja na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo





Na Anna Titus
Kukosekana kwa ofisi ya Serikali za Mitaa Igunga Kunashusha Hadhi ya Kuwa Wilaya
“Ni aibu kwa Wilaya yenye zaidi ya miaka 40 kukosa ofisi za Serikali ya Mtaa”
KATIBA  ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania inafafanua kuwa Serikali za mitaa ni vyombo vya wananchi vilivyopo katika ngazi ya msingi ya serikali.Serikali za Mitaa huundwa,huendeshwa,husimamiwa na kuwajibika kwa wananchi wenyewe. Hivyo basi Serikali za mitaa zimeundwa kwa mantiki ya kuwawezesha Wananchi, wanaume kwa wanawake,kushiriki katika masuala ya siasa,uchumi,upatikanaji wa huduma na utawala katika maeneo yao na katika nchi yao.Kwa ujumla ni muundo ambao unawawezesha wananchi kuwa na udhibiti wa maamuzi ya wawakilishi waliowachagua. Kwa mtazamo huu wa kikatiba,serikali za mitaani fursa kwa wanajamii kukuza demokrasia na ushiriki wao katika maendeleo ya maeneo yao.Ni vyema ieleweke kuwa serikali za mitaa si wakala wa serikali kuu bali ni Serikali kamili zenye mamlaka chini ya sheria.Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania,Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote na serikali inapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi.Hii ndiyo maana hasa ya kupeleka madarakakwa wananchi.

Kuundwa kwa vitongoji ni mojawapo ya marekebisho yaliyofanywa siku za karibuni ili kuboresha muundo wa serikali za Mitaa.Lengo la serikali la kuanzisha vitongoji ni pamoja na kuimarisha demokrasia kwa wananchi,na kuziba pengo lililoachwa baada ya kuondolewa wajumbe wa Nyumba kumikumi waliokuwa chini ya mfumo wa chama kimoja cha kisiasa.Kuwepo kwa vitongoji kunatoa fursa kwa wananchi kushiriki kimoja katika siasa ya vyama vyingi kwa ngazi ya msingi kabisa.Ni jambo la kawaida kukuta kuwa wenye viti wa vitongoji mbalimbali katika kijiji kimoja wanatoka kwenye vyama tofauti vya siasa.
Katika hali ya kushangaza Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora ni moja kati ya Wilaya kubwa katika mkoa huo lakini cha kushangaza ni kukosekana kwa ofisi ya serikali za mitaa kama ilivyo sehemu nyingine.
Abdalah Said ni mwenyekiti wa mtaa wa Stoo ya Pamba anasema,wilaya hiyo ilianzishwa Mwaka 1975 na mwaka 1976 ndipo ulifanyika uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mitaa. Lakini mpaka hivi leo katika wilaya hiyo hakuna kitu kinachoitwa ofisi ya Serikali za mitaa.
“sisi wenyeviti tunashindwa kufanya kazi kwa kuweka kumbukumbu za taarifa za wananchi kwa usahihi kutokana na kukosekana kwa ofisi hizo,shughuli zote tunafanyia majumbani kwenu yani katika makazi tunayoishi na familia zetu ndipo ofisi zilipo,hivyo kwa kukosa ofisi ya kuendeshea shughuli inapelekea sisi kukosa kumbukumbu stahiki na sahihi zinazoonyesha uhalali wa wanannchi”anasema.
Aliongeza kuwa vifaa vyote vya ofisi vinakaa nyumbani kitu ambacho si salama na hakileti tija ya uongozi kwani kazi za ofisini ni tofauti na kazi za nyumbani na ndio maana maofisi yote hukaa mbali na nyumbani kwa ajili ya kuepusha adha na usumbufu mbalimbali ambao kwa namna moja ama nyingine yaweza kuwa ni tatizo.
Aidha Mwenyekiti huyo alisema, “tangu mwaka 2010 tuliahidiwa kuanzishwa kwa mji mdogo na ofisi zitajengwa lakini tangu mwaka huo hakuna kinachoendelea,tumekuwa watu wa kupewa ahadi hewa kila kukicha hata karatasi kwa ajili ya shughuli za kiofisi tumekuwa tukijinunulia wenyewe. Mfano wagonjwa wenye msamaha hatuna karatasi maalumu kwa ajili ya kuwapa kwenda kutibiwa zaidi ya kuchana katika daftari na kumwandikia je kumbukumbu ziko yapi?”
Alisema kuwa,wao kama wenyeviti wanafanya kazi katika mazingira magumu na hawana msaada wowote,ila kappa wakipata ofisi ufanisi wao wa kazi utaongezeka zaidi.

Wakati naendelea kufanya mazungumzo na mwenyekiti huyo nilishuhudia mwanamke mmoja ambaye mwanae aligongwa na gari hivyo alikuja kwa ajili ya kuulizia kesi yake inaendeleaje.
Kwa upande wake mmoja wa wakazi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Masanja alisema,hiyo kama wilaya haistahili kuwa hivyo ilivyo na badala yake serikali inatakiwa iboreshe kwani maendeleo yanaanzia chini.ofisi ya serikali za mitaa ina maana kubwa sana kwani ndio mahala pekee ambapo unaweza kupata kumbukumbu za wakazi wa eneo husika.
“unajua kama kungekuwa hakuna umuhimu wa ofisi nadhani hakuna mtu yeyote ambaye angetoka asubuhi na kwenda katika ofisi flani sisi wananchi tunapata shida sana kutokana na kuwa mimi nimepata tatizo lakini tatizo langu sitaki mtu mwingine ajue zaidi ya kiongozi wangu lakini ninapokwenda kwa mwenyekiti nakuta na familia yake ipo nawezaje kuzungumza waziwazi huku familia yake ikinisikiliza? Ifike mahali serikali itambue umuhimu wa hawa viongozi wa chini kwani bila hawa wao bado hawajawa viongozi wan chi nzima ifikie kipindi watambue mchango wao ni upi katika jamii”anasema Bw.Masanja

Naye Bi.Ashura Ramadhan alisema wao wamekwisha zoea hali hiyo na wanaona ni kawaida tu kwenda kwa mwenyekiti na kuelezea matatizo yako japokuwa si vyema lakini hii inatokana na utendaji mbovu hasa wa mbunge wa jimbo hilo lenye zaidi ya miaka 40
“sisi kama wananchi hali hii inakera sana kiukweli kwa sababu mimi si mzaliwa wa hapa huko nilikotoka mambo kama haya hayakuwepo kama ukipata shida ya kwenda kwa Mwenyekiti ni lazima utaenda katika ofisi yake na si nyumbani,ikitokea umekwenda nyumbani ujue hiyo ni dharura au muda wa kazi umekwisha hivyo itakulazimu uende nyumbani kwakwe. Lakini huku nyumba ya mwenyekiti ndio ofisi ya Serikali ya Mtaa hadhi na heshima ya ofisi iko yapi?”alisema.
Majukumu ya Serikali za Mitaa yanaangukia katika sehemu kuu nne ambazo kuwezesha na kudumisha utulivu, amani na utawala bora, Kudumisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii na miundo mbinu,Kuchochea maendeleo ya kiuchhummi na kijamii na Kulinda mazingira kwa lengo la la kuchangia katika maendeleo endelevu.
Utekelezaji wa majukumu haya unategemea jinsi ambavyo ngazi mbalimbali katika serikali za mitaa zinavyotekeleza wajibu na majukumu katika mfumo wote wa serikali za mitaa ili kuongeza ufahamu miongoni mwa wananchi.
Pamoja na kuwepo kwa majukumu ya serikali za mitaa haya pia ni majukumu ambayo wananchi wanatarajiwa kuyatekeleza, Kisheria na kiutawala wananchi wanatarajiwa kutekeleza majukumu yafuatayo:kuelewa Sheria zote zinazohusu serikali za Mitaa na kuishi kufuatana na sheria hizo,Kutambua nafasi yake katika jamii na kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo, Kudai haki zake za msingi kutoka kwa viongozi wake,kuhakikisha kuwa viongozi wanatimiza wajibu wao kama ipasavyo.




Lakini kwa majukumu haya ambayo Serikali za mitaa bila kuwa na ofisi wananchi watazijuaje haki zao?


                                         
KITUO CHA HALI YA HEWA
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la ICIPE-CHIESA kutoka nchini Kenya, Dkt. Tino Johnson (wa pili kushoto), akikabidhi mtambo wa kituo cha hali ya hewa kilichojengwa kwa msaada wa Serikali ya Finland kwa ajili ya Mamlaka ya Hali ya Hewa, mkoani Kilimanjaro. Kulia ni mmoja wa wadau, Ruben Mashingia Kirua Vunjo Magharibi na Mtalaamu wa mambo ya maji wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa David Mwakalila. (Na Mpigapicha Wetu)

         Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda akiwaongoza madiwani wa manispaa hiyo wakati wa maziko ya Diwani wa Mbweni Bw.Boniface Nyachibwe yaliyokuwa mwishoni mwa wiki. Picha Charles Lucas

 Mkazi wa Mbagala akchagua mafungu ya Zabibu zilizopangwa chini bila kujali afya yake katika barabara ya Kilwa,Mbagala kama alivyokutwa Dar es Salaam jana
Baadhi ya magari yakiwa yameegeshwa nje ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT), Azania Front Posta jana, Dar es Salaam kutokana na tatizo la maaegesho. (Picha na Charles Lucas
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bw. Tom Borghols (kushoto), akipeana mkono na Mkurugenzi wa Kampuni ya MIC Tanzania Limited 'TIGO', Bw. Ruan Swanepoel, mara baada ya kutiliana saini mkataba, Dar es Salaam hivi karibuni ambapo wateja watapata huduma za uhamishaji kifedha katika taasisi hizo. Kushoto ni Mkuu wa Kutengo cha Wateja Huduma Binafsi, Abdul Nsekela. (Picha na Charles Lucas)

 Baadhi ya wakazi na watoto wa Jiji la Dar es Salaam, wakiwa katika matembezi ya hiari ya Kilometa 9, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Saratani Duniani yaliyolenga kuongeza ufahamu kwa jamii kuhusu dalili za awali za  Saratani ya watoto, yaliyoandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Tumaini la Maisha Tanzania (TMT) kwa Kushirikiana na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji  wa hospitali hiyo, Dkt. Marina Njelekela na Katikati ni Mkurugenzi wa shirika hilo. Janet Mbuguni. (Picha na Charles Lucas

                     

No comments:

Post a Comment