Friday, March 14, 2014

' KWANINI UENDE BAR IKIWA HUNA FEDHA ? '



                   KAURI YA LEO  SEHEMU YA 1
   
                    ‘Tutafakari pamoja’

‘Kwanini Uende Bar  ikiwa huna fedha’ ?
Ndugu wapenzi na watazamaji na wasomaji  wa Mtandao wa Umojamatukio nikiwa founder wa mtandao huu nimetafakari nikaona kuna umuhimu wa kuwapo kwa koramu itakayosaidia kurekebisha tabia zetu kwa msaada wa pamoja kama jamii lengo kuu likiwa ni Kuburudisha Kuelimisha na Kutahadharisha kwa manufaa ya jamii yetu.

‘Kwa leo tunaanza kwa tafakari hii katikati head line hapo juu.’ Kwanini uende bar au katika stare ilhali huna fedha’,  karibuni tuendelee
Kumemekuwapo na baadhi ya watu wenye tabia inayoelekea kuchosha na kusumbua wengine  hivi karibuni nikiwa katika mizunguko mbalimbali ya kimaisha nilikumbana na kituko cha mtu aliyeonekana kama ni mtu mstaarabu lakini cha ajabu aliingia katika Bar huko Mbagala na kuketi kwenye kona kana kwamba anamsubiri mtu huku akiwa na chupa ya maji yaliyokuwa yakikaribia kumalizika.

Lakini jambo la ajabu mtu Yule alikuwa akiangazamithili ya mtu anayemsaka mbaya wake la hasha ! kumbe alikmuwa akitafuta mfadhili wa kinywaji lo ?! kilichonishangaza ni ujasili wa mtu Yule kuomba pombe katika mazingira yale ambayo kwa kawaida  kila anayekaribia huwa amejipanga kwa bajeti yake.

Na kibaya zaidi nilichokiona kwanini? ikiwa hana fedha awahi mapema bar kabla wenye nazo hawajafika
katika hali ya kawaida ni fedheha kuomba pombe kwani si kitu cha kipaumbele kwa kuishi kama kilivyo chakula watu hawa hunoa ndimi za kinafiki kwa kujifanya wakiwasifu kwa maneno ya ghiriba wenye nazo ili waonewe huruma hiyo ni aibu.

Kundi la watu wa aina hii ni wengi wengine ni jirani zako wengine ni ndugu zetu basi naomba tutafakari kwa makini kauri yetu ya leo kisha tuchukue hatua ya tujirekebishe kwanini tuwasumbue wenye nazo ilhali hawakutuita kwenda kwenye starehe.

                   Aksanteni sana subiri neon la kesho

                  Changia maoni charleslucas800@yahoo.com  
                        0755 851441/ o718 138527



No comments:

Post a Comment