KAURI YA LEO SEHEMU YA 1
‘Tutafakari pamoja’
‘Kwanini Uende
Bar ikiwa huna fedha’ ?
Ndugu wapenzi na
watazamaji na wasomaji wa Mtandao wa
Umojamatukio nikiwa founder wa mtandao huu nimetafakari nikaona kuna umuhimu wa
kuwapo kwa koramu itakayosaidia kurekebisha tabia zetu kwa msaada wa pamoja
kama jamii lengo kuu likiwa ni Kuburudisha Kuelimisha na Kutahadharisha kwa
manufaa ya jamii yetu.
‘Kwa leo tunaanza
kwa tafakari hii katikati head line hapo juu.’ Kwanini uende bar au katika
stare ilhali huna fedha’, karibuni
tuendelee
Kumemekuwapo na
baadhi ya watu wenye tabia inayoelekea kuchosha na kusumbua wengine hivi karibuni nikiwa katika mizunguko
mbalimbali ya kimaisha nilikumbana na kituko cha mtu aliyeonekana kama ni mtu
mstaarabu lakini cha ajabu aliingia katika Bar huko Mbagala na kuketi kwenye
kona kana kwamba anamsubiri mtu huku akiwa na chupa ya maji yaliyokuwa
yakikaribia kumalizika.
Lakini jambo la
ajabu mtu Yule alikuwa akiangazamithili ya mtu anayemsaka mbaya wake la hasha !
kumbe alikmuwa akitafuta mfadhili wa kinywaji lo ?! kilichonishangaza ni
ujasili wa mtu Yule kuomba pombe katika mazingira yale ambayo kwa kawaida kila anayekaribia huwa amejipanga kwa bajeti
yake.
Na kibaya zaidi
nilichokiona kwanini? ikiwa hana fedha awahi mapema bar kabla wenye nazo
hawajafika
katika hali ya
kawaida ni fedheha kuomba pombe kwani si kitu cha kipaumbele kwa kuishi kama
kilivyo chakula watu hawa hunoa ndimi za kinafiki kwa kujifanya wakiwasifu kwa
maneno ya ghiriba wenye nazo ili waonewe huruma hiyo ni aibu.
Kundi la watu wa
aina hii ni wengi wengine ni jirani zako wengine ni ndugu zetu basi naomba
tutafakari kwa makini kauri yetu ya leo kisha tuchukue hatua ya tujirekebishe
kwanini tuwasumbue wenye nazo ilhali hawakutuita kwenda kwenye starehe.
Aksanteni sana subiri neon
la kesho
Changia maoni
charleslucas800@yahoo.com
0755 851441/ o718
138527
No comments:
Post a Comment