Friday, March 14, 2014

TUTAFAKARI PAMOJA KAURI YA LEO







           KAURI YA LEO  SEHEMU YA 2
             
 ‘KWANINI UOMBE KAZI KISHA UWANUNIE UNAOWAHUDUMIA’ ?!’
               
                   ‘Tutafakari pamoja’



Ndugu mpenzi Mtazamaji na msomaji wa ukurasa huu au koramu hii ya Mtandao wa Umojamatukio Blog karibu kwa mara nyingine katika Tafakari ya Leo ikiwa ni sehemu ya pili 
ya mfurulizo wa tafakari ya kila siku, leo tutajikita katika kero nyingine inayohusu jamii inayotokana na wahudumu au baadhi ya watumishi katika sekta mbalimbali zikiwamo sekta za Umma na binafsi. Karibu

Katika nchi yetu limekuwa si jambo geni kukumbana na vituko unapokwenda katika ofisi au mahala pa kupata huduma iwe ya kibiashara au huduma ya kijamii ikiwamo huduma za afya na nyinginezo.

Baadhi ya wahudumu katika maofisi utawakuta wakiwa hali ya kununa hata ukashindwa kuelewa hali hiyo inatokana na tatizo gani ilhali wewe mhudumiwa ndiyo mara ya kwanza kufika katika ofisi hiyo !

Kama hiyo haitoshi utawakuta wakiwa katika mazungumzo yasiyokoma hata unapojaribu kuwajulia hali huonekana kutokujali wala kustuka kuwa kuna mgeni na kibaya zaidi ikihitaji msaada hutoa lugha ya ukali isiyo ya kiungwana kana kwamba hawana jukumu ndani ya ofisi husika ‘Unaniangalia kwani mimi ndiyo nilikusababishia huo ugonjwa si uliupata kwa kiherehere chako’ mfano moja ya majibu katika baadhi ya hospitali za Umma, najiuliza tena kwanini Uombe kazi tena muda mrefu wa kufuatia ajira hiyo kisha uje uwanunie unaowahudumia’.

Katika eneo jingine hata ofisi binafsi kumeingia kero hii unafika kupata huduma ambayo wameiombea leseni serikalini kwa ahadi kuwa watawahudumia wateja wao (wananchi) kwa ukamirifu lakini kinachotokea ni usumbufu usio jali masharti ya leseni inayoruhusu kufanya biashara au huduma husika,

Moja ya mifano ni katika baadhi ya mabenki utakuta vidilisha vya huduma (Tillers) vikiwa zaidi ya 10 lakini cha ajabu ni vidisha viwili tu kama si kimoja kinachotoa huduma !!.. hapo unajiuliza hali hiyo inayosababisha msululu wa wateja ndani ya benki husika una tija gani kwao ? unakosa jibu na kubwa zaidi utakuta wahudumu hao wakionekana kuzunguka huku wakiwa hawajali usumbufu wanaosababisha, najiuliza tena kwanini Uombe kazi kasha uwanunie na kuwasumbua unaowahudumia ? Tutafakali pamoja

             Aksanteni sana subiri neo la kesho

                  Changia maoni charleslucas800@yahoo.com  
                        0755 851441/ 0718 138527






KAURI YA LEO  SEHEMU YA 1
  ‘Tutafakari pamoja’

‘Kwanini Uende Bar ikiwa huna fedha’ ?

Ndugu wapenzi na watazamaji na wasomaji  wa Mtandao wa Umojamatukio nikiwa founder wa mtandao huu nimetafakari nikaona kuna umuhimu wa kuwapo kwa koramu itakayosaidia kurekebisha tabia zetu kwa msaada wa pamoja kama jamii lengo kuu likiwa ni Kuburudisha Kuelimisha na Kutahadharisha kwa manufaa ya jamii yetu.

‘Kwa leo tunaanza kwa tafakari hii katikati head line hapo juu.’ Kwanini uende bar au katika stare ilhali huna fedha’,  karibuni tuendelee

Kumemekuwapo na baadhi ya watu wenye tabia inayoelekea kuchosha na kusumbua wengine  hivi karibuni nikiwa katika mizunguko mbalimbali ya kimaisha nilikumbana na kituko cha mtu aliyeonekana kama ni mtu mstaarabu lakini cha ajabu aliingia katika Bar huko Mbagala na kuketi kwenye kona kana kwamba anamsubiri mtu huku akiwa na chupa ya maji yaliyokuwa yakikaribia kumalizika.

Lakini jambo la ajabu mtu Yule alikuwa akiangazamithili ya mtu anayemsaka mbaya wake la hasha ! kumbe alikmuwa akitafuta mfadhili wa kinywaji lo ?! kilichonishangaza ni ujasili wa mtu Yule kuomba pombe katika mazingira yale ambayo kwa kawaida  kila anayekaribia huwa amejipanga kwa bajeti yake.

Na kibaya zaidi nilichokiona kwanini? ikiwa hana fedha awahi mapema bar kabla wenye nazo hawajafika
katika hali ya kawaida ni fedheha kuomba pombe kwani si kitu cha kipaumbele kwa kuishi kama kilivyo chakula watu hawa hunoa ndimi za kinafiki kwa kujifanya wakiwasifu kwa maneno ya ghiriba wenye nazo ili waonewe huruma hiyo ni aibu.

Kundi la watu wa aina hii ni wengi wengine ni jirani zako wengine ni ndugu zetu basi naomba tutafakari kwa makini kauri yetu ya leo kisha tuchukue hatua ya tujirekebishe kwanini tuwasumbue wenye nazo ilhali hawakutuita kwenda kwenye starehe.

                   Aksanteni sana subiri neon la kesho

                  Changia maoni charleslucas800@yahoo.com  
                        0755 851441/ o718 138527



No comments:

Post a Comment