Saturday, May 31, 2014

TBL YAFUATA TUZO ZA MONTE SELECTION UFARANSA NI ZA UBORA WA BIA ZAKE

Meneja wa Bia ya Safari Lager wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Oscar Sherukindo (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, kabla ya kuondoka kwenda Ufaransa kuchukua Tuzo ya Kimataifa ya Monde Selection iliyotunukiwa bia hiyo kutokana na ubora. Kulia ni Meneja wa Bia ya Ndovu Pamela Kikuli ambayo pia imepata tuzo hiyo na Mpishi Mkuu wa bia hizo, Calvin Nkya.
Warembo Prisca Clement (kulia) na Sion Fransis wakiwa na vikombe vilivyotwaliwa na TBL kwa ubora wa vinywaji vyake, wakati wakiwasindikiza mameneja walipokuwa wakienda Ufaransa
Mameja wa Safari Lager na Ndovu na Mpishi Mkuu wa Bia wakiwa na mabegi yao kabla ya kuondoka. Kutoka Kushoto, Oscar Sherukindo Safari Lager Mpishi Mkuu wa bia hizo Calvin Nkya na Meneja wa Ndovu, Pamela Kikuli
                         Warembo wakipoozi na vikombe vya TBL uwanja wa Ndege Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment